Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Claim This Podcastby United Nations
Podcast Overview
Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Language
🇸🇼
Publishing Since
2/12/2024
1 verified contact email on file for Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Pitch yourself as a guest, propose sponsorships, or reach out directly to the host.
Recent Episodes

June 18, 2026
18 JUNI 2026
<p>Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina. Katika mkutano wa 19 wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Haki za Watu Wenye Ulemavu uliomalizika wiki iliyopita baadhi ya wahudhuriaji walikuja na wakalimani wao, kutoka Tanzania Mbunge Nassriya Nassir Ali mwenye ulemavu wa kusikia au Kiziwi aliambatana na mkalimani wake Tusajigwe Ernest. </p><p>Baada ya mkutano huo Leah Mushi aliketi na Tusajigwe na hapa anaanza kwa kueleza kuhusu taaluma yake. Pia tunakuletea muhtasari wa habari.</p><ol><li>Kauli za chuki zinaendelea kuhatarisha mshikamano wa jamii na amani duniani, ameonya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres akisema mara nyingi ndizo chachu ya vurugu, migogoro na uhalifu mkubwa dhidi ya ubinadamu. Katika ujumbe wake wa Siku ya Kimataifa ya Kupambana na Kauli za Chuki, leo Juni 18, Guterres amesema makundi kama wanawake, wahamiaji, wakimbizi, watu wenye ulemavu na jamii ya LGBTQIA+ mara nyingi hulengwa na ujumbe wa chuki. “Kauli za chuki ndio hatua ya kwanza katika njia ya kuwanyima watu utu wao, njia ambayo mara nyingi hupelekea vurugu, migogoro na uhalifu wa kutisha.” Pia ameonya kuwa mitandao ya kijamii imeongeza kasi ya kusambaa kwa chuki duniani.</li><li>Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda Amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, MONUSCO, umetangaza kwa masikitiko hii leo kifo cha mfanyakazi wa kampuni iliyokuwa ikitoa huduma kwa ujumbe huo, aliyefariki dunia kutokana na Ebola mjini Bunia. MONUSCO imesema mfanyakazi huyo alikuwa ameacha kufanya kazi na ujumbe huo tangu Mei 22 mwaka huu na hakuwa amefika katika maeneo ya MONUSCO kwa zaidi ya siku 21 kabla ya ugonjwa huo kuthibitishwa. Ujumbe huo umetuma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, marafiki na wafanyakazi wenzake na marehemu.</li><li>Na Shirika la Umoja wa Mataifa la Hali ya Hewa Duniani, WMO, limesema matukio mabaya ya hali ya hewa na mabadiliko ya tabianchi yaliathiri takriban watu milioni 13 barani Afrika mwaka 2025 na kusababisha vifo zaidi ya watu 3,000. Ripoti mpya ya shirika hilo iliyotolewa leo mjini Geneva Uswisi inaeleza kuwa mafuriko yalikuwa janga lililoripotiwa zaidi, huku yakisababisha hasara kubwa za kiuchumi na kibinadamu. WMO pia imeonya kuwa barafu katika maeneo ya milima ya Afrika, ikiwemo Mlima Kilimanjaro, inaendelea kutoweka kwa kasi, wakati kina cha bahari katika baadhi ya maeneo ya pwani kikipanda kwa kiwango kikubwa kuliko wastani wa dunia. WMO imesisitiza kuwa Afrika bado ina pengo kubwa katika mifumo ya tahadhari za mapema, ingawa maendeleo yanaendelea kufanyika.</li></ol><p>Mwenyeji wako ni Feissal Kirwa, karibu!</p>

June 17, 2026
Vijana wanahitaji ajira, stadi na matumaini bila hivyo, ni rahisi kutumbukia kwenye uhalifu - Monica Juma
<p>Wakati dunia ikikabiliwa na ongezeko la uhalifu wa kupangwa, biashara haramu ya binadamu na matumizi ya dawa za kulevya, mwanamke kutoka Afrika Mashariki amepewa jukumu kubwa la kusaidia kuongoza mapambano ya kimataifa dhidi ya changamoto hizo. </p><p>Monica Juma, ambaye hivi karibuni ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Dawa za Kulevya na Uhalifu (<a href="https://www.unodc.org/" target="_blank" title="(opens in a new window)" data-extlink>UNODC</a>), anavunja rekodi kwa kuwa mwanamke wa kwanza kutoka Afrika Mashariki na Kusini mwa dunia kushika nafasi hiyo ya juu katika taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa. </p><p>Pata mahojiano maalum na ya kina baina ya Flora Nducha wa Idhaa hii na Mkuu huyu mpya wa ofisi ya UNODC.</p>

June 17, 2026
Watoto 9 waliotumikishwa kijeshi na waasi waachiwa na kuanza maisha mapya nchini Sudan Kusini
<p>Watoto tisa waliokuwa wakihusishwa na vikosi vya ulinzi katika Jimbo la Equatoria Magharibi nchini Sudan Kusini wameanza safari mpya ya maisha baada ya kutambuliwa, kuachiliwa na kukabidhiwa kwa ajili ya kurejeshwa katika familia na jamii zao.</p>
1,717 total episodes available
Recent guests on Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Guests from recent episodes — sign up to see every guest that has ever appeared on this show.
Abeida Rashid Abdallah
Guest
Jescah Muyia
Guest
Onni Sigalla
Guest
Sharon Jebichii
Guest
Natalia Toschi
Guest
Anold Kayanda
Guest
Deep-dive analytics for Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
Frequently asked questions
Have a different question and can't find the answer you're looking for? Reach out to our support team by sending us an email and we'll get back to you as soon as we can.
- What is Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu?
- How often does this podcast release new episodes?
This podcast updates daily.
- Where can I listen to this podcast?
This podcast is available on 8 platforms including Apple Podcasts, Spotify, and more. You can also use the RSS feed directly.
- Does this podcast accept guests?
Yes, this podcast regularly features guests.
Legal Disclaimer
Pod Engine is not affiliated with, endorsed by, or officially connected with any of the podcasts displayed on this platform. We operate independently as a podcast discovery and analytics service.
All podcast artwork, thumbnails, and content displayed on this page are the property of their respective owners and are protected by applicable copyright laws. This includes, but is not limited to, podcast cover art, episode artwork, show descriptions, episode titles, transcripts, audio snippets, and any other content originating from the podcast creators or their licensors.
We display this content under fair use principles and/or implied license for the purpose of podcast discovery, information, and commentary. We make no claim of ownership over any podcast content, artwork, or related materials shown on this platform. All trademarks, service marks, and trade names are the property of their respective owners.
While we strive to ensure all content usage is properly authorized, if you are a rights holder and believe your content is being used inappropriately or without proper authorization, please contact us immediately at hey@podengine.ai for prompt review and appropriate action, which may include content removal or proper attribution.
By accessing and using this platform, you acknowledge and agree to respect all applicable copyright laws and intellectual property rights of content owners. Any unauthorized reproduction, distribution, or commercial use of the content displayed on this platform is strictly prohibited.
