Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran

Iran-Tanzania Podcast
Claim This Podcastby Iran.Tanzania
Podcast Overview
Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
Language
🇸🇼
Publishing Since
5/19/2021
1 verified contact email on file for Iran-Tanzania Podcast
Pitch yourself as a guest, propose sponsorships, or reach out directly to the host.
Recent Episodes

April 21, 2022
MALENGA WA KIIRANI SAADI SHIRAZI
Musharraf al-Din Mosleh ibn Abdullah ibn Musharraf, ambaye baadaye alijulikana kama Saadi Shirazi, ni mmoja kati ya malenga na mshairi mkubwa na mashuhuri nchini Iran. Wanahistoria wanaamini kwamba Saadi Shirazi alizaliwa kati ya mwaka 600 na 610 Hijiria (sawa na takriban mwaka 1210 Miladia). Walakini, hakuna tarehe kamili inayojulikana ya kuzaliwa kwa malenga huyu, ingawa wanahistoria wanakadiria mwaka huo wa kuzaliwa kulingana na athari za kazi zake. Saadi alizaliwa katika familia ya wanazuoni, wasomi na watu wenye maadili mema. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa Mahakama ya Atabak na Shah Saad bin Zangi. Wengine wanaamini kwamba mshairi huyu amechagua jina la ukoo la Saadi kama ni mtu mwenye utambuzi wa haki. Mbali na kuhudumu katika mahakama, baba yake pia alikuwa akijishughulisha na masuala ya kidini na alikuwa akimshajiisha mno mtoto wake kujifundisha elimu ya kisekula na kidini pia. Kwa msaada wa baba yake, Saadi alipata ujuzi wa kina katika nyanja za historia na fasihi. Wakati wa kuzaliwa kwake, mtawala wa Shiraz alikuwa mfalme wa tatu wa serikali ya Atabakan. Nguvu ya Waseljuk ilipodhoofika siku baada ya siku katika kutawala nchi, uliibuka mlolongo wa utawala wa kieneo. Mbali na Shiraz, Atabak pia alikuwa na nguvu za kiutawala huko Damascus, Mosul, Aleppo (Halab), Mesopotamia ( Furati na Hidekeli), na Azerbaijan. Baba yake Saadi alifariki dunia, wakati Saadi akiwa na umri wa miaka 12, na babu yake mzaa mama, Massoud ibn Mosleh, alichukua jukumu la kumlea na kumtunza mjukuu wake. Katika wasifu wa Saadi, tunasoma kwamba baada ya mshairi huyu kujifunza misingi ya elimu ya kidini na fasihi huko Shiraz, alikwenda Baghdad akiwa bado barobaro na kijana chini ya usimamizi wa Atabak na akajiunga katika madrasa ya Nidhamiyyah. Shule hii ilikuwa inatoa elimu maalumu kwa watu wanaotaka kujikita zaidi katika nyanja za fiqh ( sheria za Kiislamu) na falsafa. Wanazuoni wakubwa kama vile Suhrawardi walimlea kielimu Saadi katika madrasa hiyo. Baada ya kumaliza mafunzo, Saadi akaazimia kufanya safari katika maeneo ya Hijaz, Sham na Syria kwa lengo la kupata elimu na uzoefu zaidi. Baada ya hapo akashika njia na kuelekea Makka. Wakati huo huo, alifanikiwa kufunga ndoa, na kisha alifanikiwa kupata mtoto, lakini baada ya kumpoteza mtoto wake huyo, Saadi aliamua kusafiri tena ili kuvumilia mateso hayo, mateso ambayo yalimfanya awe mwenye kupenda zaidi mashairi. Saadi alitembelea miji mbalimbali duniani kote na huko alijishughulisha zaidi na kufundisha na kuhubiri katika miji hiyo. Wataalamu wengine wa historia wamethibitisha kufanya safari yake ya India na sehemu nyingine kadhaa za dunia, na wanaeleza kuwa, safari hizo zilidumu takriban miaka 30. Hata hivyo, muda wa safari na maeneo aliyotembelea Saadi, ni mambo ambayo bado yanatiliwa shaka mno. Hatimaye, baada ya kupita miaka mingi na kupata uzoefu wa kutosha, malenga huyu aliamua kurudi katika nchi yake na mji wake wa asili wa Shiraz. Wakati wa kurejea kwake Shiraz, Abu Bakr ibn Sa'd, mfalme wa Atabaki, alikuwa akitawala huko Shiraz wakati huo. Na kulingana na baadhi ya maelezo ya watu, mshairi huyo alichukua jina la ukoo wa Saadi kutoka kwa jina la mfalme (Saad). Baada ya Saadi kurejea Shiraz, mshairi huyu alianza kuandika na kukusanya kazi zake. Kazi yake ya kwanza aliyoiandika ilikuwa kuandika kitabu cha mashairi alichokipa jina la Bustan, mnamo mwaka 655 Hijria, na kukabidhi mkusanyiko wa mashairi hayo kwa mfalme aliyekuwa akitawala kipindi hicho aitwaye Abubakar ibn Sa'd Zangi. Kitabu cha mashairi cha Golestan kilichoandikwa na malenga huyu mkubwa kilitungwa mwaka wa 656 Hijiria, mwaka mmoja baada ya kuandikwa kwa kitabu cha Bustan. Saadi alikamilisha uandishi wa mashairi ya kitabu hicho kwa muda mfupi. Kuandikwa kwa vitabu viwili katika muda mfupi kunaonyesha kwamba, kwa kiasi kikubwa mashairi hayo yalikuwa yameshatayarishwa mapema, bali alichokifanya ni kukusanya na kufanya masahihisho katika hatua za mwisho kabla ya kuchapishwa. Mengi yamesemwa kuhusu Saadi juu

April 18, 2022
ATTAR NEYSHABURI MALENGA WA KIIRANI
<p>ATTAR NEYSHABURI MALENGA WA KIIRANI</p> <p> </p> <p>Tarehe 25 Farvardin kwa mujibu wa ( Kalenda ya Kiirani) inayosadifiana na tarehe 14 Aprili, ni siku ya kumkumbuka na kumuadhimisha malenga wa Kiirani Farid al-Din Abu Hamid Muhammad bin Abu Bakr Ibrahim bin Is- haq Attar Neyshabouri, ambaye ni mmoja wa washairi mashuhuri, aaref na mwanafikra mkubwa wa Kiirani aliyeishi mwishoni mwa karne ya sita na mwanzoni mwa karne ya saba Hijria. Baadhi ya wanahistoria wameandika kuwa, mwanafikra na malenga huyo wa Kiajemi amezaliwa mwaka 513 na wengine wanaeleza kuwa alizaliwa mwaka 537 Hijiria. </p> <p>Attar Neyshabouri alizaliwa katika kijiji cha Kadkan au Shadiakh, ambacho wakati huo kilikuwa sehemu ya jiji la Neyshabour. Hakuna habari inayoelezea taarifa zake za utotoni mwake, isipokuwa baba yake aliishi katika mji wa Shadiakh akifanya kazi ya kuuza dawa za asili, na alikuwa mahiri na hodari mno katika biashara hii ya kuuza dawa za asili, na baada ya kufariki dunia baba yake, Farid al Din Attar Neyshabouri aliendeleza shughuli za marehemu baba yake ya kuuza dawa za asili. Wakati akishughulika na uuzaji wa dawa za asili Attar Neyshabouri alikuwa akitoa tiba ya asili na wala haijulikani utaalamu huo wa kutoa tiba ya asilii aliupata kutoka kwa nani. Attar Neyshabouri aliendelea na shughuli zake za kutoa tiba ya asili sanjari na kuuza dawa za asili hadi pale yalipopatikana mapinduzi ya kiroho na kimaanawi kwa upande wake, na jambo hili limebainishwa kwa kutolewa visa kadhaa, lakini kisa maarufu ni hiki kifuatacho:</p> <p> “Siku moja Attar Neyshabouri alikuwa dukani kwake akifanya shughuli zake, mara akaingia “Darwesh" na akaanza kusema maneno kadhaa yanayohusiana na Mwenyezi Mungu, ili Attar aweze kuvutika na kumsaidia, lakini Darwesh hakupata msaada wowote kutoka kwa Attar Neyshabouri. Darwesh akamwambia Attar : Ewe kijana unataka ufariki duniani kwa kifo cha namna gani? Attar akajibu: Kwa njia ileile ambayo wewe unataka kufa. Darwesh akasema; Wewe unataka kufa kama nitakavyokufa mimi? Attar akajibu: Ndio, Darwesh akachukua bakuli lake lililotengenezwa kwa mbao na kuliweka chini ya kichwa chake na akasema maneno ya Mwenyezi Mungu na hatimaye kufariki dunia. Kwa vile Attar Neyshabouri aliliona tukio hilo kwa macho yake aliathirika mno na kubadilika na akaamua kutoka dukani na kubadilisha kikamilifu mtindo na mwenendo wa maisha yake” .</p> <p>Attar Neyshabouri aliposhuhudia tukio hilo la Darwesh , akaacha kabisa shughuli za tiba na biashara za dawa za asili, na akaamua kuelekea kwa Sheikh Mkuu Aref Rukniddin Akaf , wakati huo Sheikh Aref alikuwa mtu maarufu na mashuhuri mno na kwa miaka kadhaa Attar Neyshabouri alikuwa akipata elimu na maarifa kutoka kwa sheikh Aref Rukniddin Akaf. </p> <p>Attaf Neyshabouri aliweza kutumia nusu ya umri wake kwa kufanya safari katika miji mbalimbali, na katika safari zake hizo alifanikiwa kukutana na masheikh wakubwa wakubwa katika zama hizo, na safari hizo ziliweza kumfikisha hadi kwa sheikh Majiduddin Baghdadi. </p> <p>Inasemekana kuwa Sheikh Aref alipofikia marika ya uzee, Bahauddin Muhammad baba wa Jalaluddin Balkhi alikuwa pamoja na mwanawe walifanya safari ya kuelekea Iraq , wakiwa njiani walipitia Neyshabouri na wakafanikiwa kumtembelea Attar Neyshabouri, hivyo Sheikh Attar Neyshabouri alitoa nakala moja kati ya makala zake za mashairi na kumpa Jalaluddin ambapo wakati huo alikuwa bado kijana mdogo mno.</p> <p><br></p>

March 27, 2022
Siku kuu ya Nowruz Mwaka Mpya wa Kiiran
<p>Jumatatu ya Tarehe 21 Machi 2022 Miladia inayosadifiana na tarehe (Mosi / Farvardin 1401) ni siku ya kuanza mwaka mpya wa Kiirani wa Hijria Shamsia. Siku hii ambayo hujulikana kama <strong>Nowruz</strong>, ni mwanzo wa sherehe za kale na za muda mrefu na matawi yake yameenea katika kona mbalimbali za Dunia hadi Afrika Mashariki. Asili ya sherehe za <strong>Mwaka Kogwa </strong>huko Makunduchi visiwani Zanzibar, ni sherehe hizo za Nowruzi za nchini Iran.</p>
12 total episodes available
Deep-dive analytics for Iran-Tanzania Podcast
Frequently asked questions
Have a different question and can't find the answer you're looking for? Reach out to our support team by sending us an email and we'll get back to you as soon as we can.
- What is Iran-Tanzania Podcast?
- How often does this podcast release new episodes?
This podcast updates daily.
- Where can I listen to this podcast?
This podcast is available on 4 platforms including Apple Podcasts, Spotify, and more. You can also use the RSS feed directly.
- Does this podcast accept guests?
Information about guest appearances is not available.
Legal Disclaimer
Pod Engine is not affiliated with, endorsed by, or officially connected with any of the podcasts displayed on this platform. We operate independently as a podcast discovery and analytics service.
All podcast artwork, thumbnails, and content displayed on this page are the property of their respective owners and are protected by applicable copyright laws. This includes, but is not limited to, podcast cover art, episode artwork, show descriptions, episode titles, transcripts, audio snippets, and any other content originating from the podcast creators or their licensors.
We display this content under fair use principles and/or implied license for the purpose of podcast discovery, information, and commentary. We make no claim of ownership over any podcast content, artwork, or related materials shown on this platform. All trademarks, service marks, and trade names are the property of their respective owners.
While we strive to ensure all content usage is properly authorized, if you are a rights holder and believe your content is being used inappropriately or without proper authorization, please contact us immediately at hey@podengine.ai for prompt review and appropriate action, which may include content removal or proper attribution.
By accessing and using this platform, you acknowledge and agree to respect all applicable copyright laws and intellectual property rights of content owners. Any unauthorized reproduction, distribution, or commercial use of the content displayed on this platform is strictly prohibited.
